Maelezo ya Chini
c Uthibitisho mmoja ni kwamba mara 19, yana ule usemi wa Kiebrania “Lile Jina,” ukiwa umeandikwa mzima au kwa ufupi. Profesa Howard aandika hivi: “Kusoma Jina la Kimungu katika hati ya Kikristo iliyonukuliwa na mwandishi Myahudi wa makala zenye ubishi ni jambo la kutokeza. Ikiwa hii ingekuwa tafsiri ya Kiebrania ya hati ya Kikristo ya Kigiriki au ya Kilatini, mtu angetazamia kupata adonai [Bwana] katika maandishi, si ufananisho wa lile jina tukufu la kimungu YHWH. . . . Jambo la kwamba aliongeza jina hilo tukufu halielezeki. Uthibitisho hudokeza kwa nguvu kwamba Shem-Tob alipokea nakala yake ya Mathayo ikiwa tayari na Jina la Kimungu katika maandishi na kwamba labda alilihifadhi badala ya kujasiri kuwa na hatia ya kuliondoa.” Biblia ya New World Translation of the Holy Scriptures—With References hutumia maandishi ya Mathayo (J2) ya Shem-Tob kuwa utegemezo wa kutumia jina la kimungu katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.