Maelezo ya Chini
a Tito alikuwa kwenye upande wa ushindi kwa wazi. Hata hivyo, hakutimiza mambo mawili aliyotaka. Aliwapa nafasi ya kujisalimisha kwa amani, lakini viongozi wa hilo jiji walikataa kwa ushupavu, na isivyoelezeka. Na hatimaye kuta za jiji zilipobomolewa, aliamuru kwamba hekalu lisiharibiwe. Hata hivyo lilichomwa kabisa! Unabii wa Yesu ulikuwa umeonyesha kwa wazi kwamba Yerusalemu lingeangamizwa kabisa na kwamba hekalu lingebomolewa kabisa.—Marko 13:1, 2.