Maelezo ya Chini
c Katika 1267, Naḥmanides aliwasili nchi iitwayo sasa Israeli. Miaka yake ya mwisho ilijawa na mambo yaliyotimizwa. Aliimarisha tena kuwapo kwa Wayahudi na kitovu cha kujifunza katika Jerusalem. Alimaliza pia maelezo juu ya Torati, vitabu vitano vya kwanza vya Biblia, na akawa kiongozi wa kiroho wa jamii ya Kiyahudi katika mwambao wa kaskazini mwa Acre, alipofia katika 1270.