Maelezo ya Chini
c Kikundi chao kilitokana na Wahasidimu, kikundi kilichotokea karne kadhaa mapema ili kushindana na uvutano wa Kigiriki. Wahasidimu walitwaa jina lao kutokana na neno la Kiebrania chasi·dhimʹ, linalomaanisha “wenye uaminifu-mshikamanifu” au “wachaji.” Labda walihisi kwamba maandiko yanayotaja “wenye uaminifu-mshikamanifu” wa Yehova yaliwahusu kwa njia fulani ya pekee. (Zaburi 50:5, NW) Wao, pamoja na Mafarisayo wa baada yao, walikuwa washupavu, walindaji wa herufi ya Sheria waliojiweka wenyewe rasmi.