Maelezo ya Chini
b Kwa kufikiria yale ambayo yalikuwa yamewekwa imara na Sheria ya Kimusa, watu fulani wameuliza jinsi Barnaba, Mlawi, alivyokuja kupata shamba. (Hesabu 18:20) Hata hivyo, lazima ijulikane kwamba, haieleweki kama hiyo mali ilikuwa Palestina au Saiprasi. Zaidi ya hilo, yawezekana kwamba ilikuwa tu kiwanja cha maziko ambacho Barnaba alikuwa amejipatia katika eneo la Yerusalemu. Hata iweje, Barnaba alitoa mali yake kuwasaidia wengine.