Maelezo ya Chini
c Mahali ambako yaelekea desturi za mazishi zitamletea Mkristo majaribu makali, wazee waweza kuwatayarisha wataka kubatizwa kwa yale ambayo huenda wakakabili baadaye. Wanapokutana na watu hao wapya ili kuzungumzia maswali katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, wazee wapaswa kukazia uangalifu vichwa, “Nafsi, Dhambi, na Kifo” na “Kuchangamana na Dini Mbalimbali.” Vichwa hivyo viwili vina maswali ambayo wazee waweza kuchagua kuzungumzia. Wazungumziapo vichwa hivyo wazee waweza kutoa habari juu ya desturi za mazishi zisizo za Kimaandiko ili mtaka kubatizwa ajue kile ambacho Neno la Mungu hutaka afanye akikabili hali kama hizo.