Maelezo ya Chini
a Usemi “kupiga teke dhidi ya michokoo” hufafanua kitendo cha fahali ambaye hujiumiza anapopiga teke fimbo yenye ncha kali ambayo imenuiwa kuendesha na kuongoza mnyama. Vivyo hivyo, kwa kuwanyanyasa Wakristo, Sauli angejidhuru mwenyewe tu, kwa kuwa alikuwa akipigana na watu waliokuwa na utegemezo wa Mungu.