Maelezo ya Chini
b Msomi Mwingereza G. R. Beasley-Murray asema hivi: “Fungu ‘kizazi hiki’ halipaswi kusababisha ugumu wowote kwa wafasiri. Ingawa ni kweli kwamba neno genea katika Kigiriki cha mapema lilimaanisha uzazi, uzao, na kwa hivyo jamii, . . . hilo mara nyingi lilitumiwa katika [Septuagint ya Kigiriki] kutafsiri neno la Kiebrania dôr, linalomaanisha umri, umri wa jamii ya kibinadamu, au kizazi katika maana ya watu walioishi wakati mmoja. . . . Katika maneno ya Yesu, neno hilo laonekana kuwa ladokeza maana mbili: kwa upande mmoja sikuzote hilo linamaanisha watu walioishi wakati mmoja naye, na kwa upande mwingine linamaanisha ule unaoeleweka kuwa uchambuzi.”