Maelezo ya Chini
a Wanapotetea Ufalme wa Mungu, Mashahidi wa Yehova hawajihusishi na siasa au kuchochea uasi dhidi ya serikali, hata katika nchi ambapo wamepigwa marufuku au wananyanyaswa. (Tito 3:1) Badala yake, wanajitahidi kusaidia watu kiroho bila kujihusisha na siasa kama vile Yesu na wanafunzi wake wa karne ya kwanza walivyofanya. Mashahidi hujitahidi kusaidia watu wanaopenda uadilifu katika jumuiya zao mbalimbali wafuate kanuni zinazofaa za Biblia, kama vile upendo wa kifamilia, unyofu, usafi wa kiadili, na mazoea mazuri ya kazi. Wao hujitahidi hasa kuwafundisha watu watii kanuni za Biblia na kutegemea Ufalme wa Mungu ambao ndio tumaini halisi la wanadamu.