Maelezo ya Chini
a Akieleza taarifa ya Paulo kwamba “upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili,” msomi wa Biblia Gordon D. Fee aandika hivi: “Katika theolojia ya Paulo sifa ya [ustahimilivu na fadhili] yaonyesha mtazamo wa Mungu kuelekea wanadamu (linganisha Rom. 2:4). Kwa upande mmoja, uvumilivu wa Mungu unaonyeshwa na jinsi anavyozuia hasira yake dhidi ya uasi wa wanadamu; kwa upande mwingine, fadhili zake zaonekana kwa jinsi anavyoonyesha sana rehema yake. Kwa hiyo ufafanuzi wa Paulo kuhusu upendo unaanza kwa ufafanuzi huu wenye maana mbili wa Mungu, ambaye kupitia Kristo ameonyesha uvumilivu na fadhili zake kuelekea wale wanaostahili kupata hukumu yake kali.”