Maelezo ya Chini
b Yehova mwenyewe huchukizwa kabisa na maovu. Kwa mfano, andiko la Waefeso 4:29 linafafanua lugha mbaya kuwa “usemi uliooza.” Neno la Kigiriki “-liooza” larejezea kihalisi tunda, samaki, au nyama iliyooza. Neno hilo linaonyesha kinaganaga jinsi tunavyopaswa kuhisi kuhusu lugha chafu au ya matusi. Vivyo hivyo, katika Maandiko mara nyingi sanamu zinaitwa “mavi.” (Kumbukumbu la Torati 29:17; Ezekieli 6:9, NW) Kama vile tunavyochukia kabisa mavi au kinyesi, ndivyo Mungu anavyochukia kabisa kila namna ya ibada ya sanamu.