Maelezo ya Chini
a ‘Tofauti kuu kati ya Yesu na Mafarisayo inaonyeshwa waziwazi na maoni yao tofauti kuhusu Mungu. Kulingana na Mafarisayo, Mungu hasa ndiye mwenye kudai; kulingana na Yesu, Mungu ni mwenye neema na huruma. Bila shaka Mafarisayo wanakubali kwamba Mungu ni mwema na ni mwenye upendo, lakini kulingana nao, sifa hizo zinaonyeshwa katika zawadi ya Torati [Sheria] na katika uwezekano wa kutimiza matakwa ya Torati hiyo. Mafarisayo waliona kwamba Torati ingeweza kutimizwa kwa kufuata mapokeo ya mdomo, yaliyokuwa na kanuni zilizofafanua sheria. Yesu aliyakataa mapokeo ya mdomo na badala yake akaikweza sheria ya upendo kwa Mungu na jirani (Mathayo 22:34-40) kuwa msingi unaofaa wa kuifafanua Sheria. Ufafanuzi wake ulipingana na wa Mafarisayo.’—The New International Dictionary of New Testament Theology.