Maelezo ya Chini
a Hapa “nyota” hazifananishi malaika halisi. Yesu hangetumia mwanadamu kuandika habari kwa ajili ya viumbe wa roho wasioonekana. Kwa hiyo, lazima “nyota” hizi ziwe zinafananisha waangalizi wa kibinadamu au wazee katika makutaniko, wanaoonwa kuwa wajumbe wa Yesu. Nyota hizo ni saba, idadi inayoonyesha ukamilifu kupatana na kiwango cha Mungu.