Maelezo ya Chini
c Nyakati za wazee wa ukoo, kila kichwa cha familia aliwakilisha mke na watoto wake mbele za Mungu, na hata kutoa dhabihu kwa niaba yao. (Mwanzo 8:20; 46:1; Ayubu 1:5) Hata hivyo, Sheria ilipotolewa, Yehova alichagua wanaume kutoka familia ya Aroni kuwa makuhani ambao wangewatolea watu dhabihu. Yaonekana waasi hao 250 hawakutaka kukubali badiliko lililofanywa katika mpango huo.