Maelezo ya Chini
a Petro alipotembelea Antiokia ya Siria, alifurahia ushirika mchangamfu pamoja na waamini wasio Wayahudi. Hata hivyo, Wakristo Wayahudi walipowasili kutoka Yerusalemu, Petro ‘alianza kujiondoa na kujitenga mwenyewe, kwa kuwahofu hao wa tabaka ya waliotahiriwa.’ Tunaweza kuwazia jinsi wageuzwa-imani hao wasio Wayahudi walivyoumia wakati mtume huyo aliyeheshimika alipokataa kula pamoja nao.—Wagalatia 2:11-13.