Maelezo ya Chini
b Ijapokuwa kuna maoni yanayotofautiana, wataalamu fulani wanatambua hekalu la Dagani kuwa ndilo hekalu la mungu Eli. Roland de Vaux, msomi wa Biblia Mfaransa katika Shule ya Yerusalemu ya Mafunzo ya Biblia, anasema kwamba Dagani, yaani Dagoni wa kitabu cha Waamuzi 16:23 na 1 Samweli 5:1-5 ni jina la kibinafsi la mungu Eli. Kitabu The Encyclopedia of Religion kinatoa maelezo haya: “Dagani alikuwa akishirikishwa au kufananishwa na [Eli].” Katika maandishi ya Ras Shamra, Baali anaitwa mwana wa Dagani, lakini maana ya neno “mwana” hapa si hakika.