Maelezo ya Chini
a Katika Maandiko, neno “chuki” lina maana mbalimbali. Katika hali fulani, neno hilo humaanisha tu kutopenda sana. (Kumbukumbu la Torati 21:15, 16) Pia, neno “chuki” linaweza kumaanisha kutopenda kitu hata kidogo lakini bila kuwa na nia ya kukidhuru, badala yake kujaribu kukiepuka kwa sababu ya kukichukia. Hata hivyo, neno “chuki” linaweza pia kumaanisha uadui mkubwa, unaoendelea kwa muda mrefu na ambao mara nyingi huhusisha uovu. Katika makala hii, tutazungumzia maana hii ya mwisho.