Maelezo ya Chini
a Kitabu La Sagrada Escritura—Texto y comentario por profesores de la Compañía de Jesús (Maandiko Matakatifu—Maandishi na Maelezo ya Maprofesa wa Shirika la Yesu) yanasema kwamba “kati ya Waajemi, Wamedi, na Wakaldayo, Mamajusi walifanyiza jamii ya ukuhani ambayo iliendeleza mambo ya uchawi, unajimu, na uganga.” Hata hivyo, kufikia Enzi za Kati, Mamajusi ambao walienda kumwona mvulana Yesu walitangazwa kuwa watakatifu na kupewa majina Melchior, Gaspar, na Balthasar. Na inadaiwa kwamba mabaki yao yamehifadhiwa katika kanisa kuu la Cologne, Ujerumani.