Maelezo ya Chini
a Mfalme Daudi wa Israeli la kale aliiteka ngome ya Mlima Sayuni wa kidunia kutoka kwa Wayebusi na kuifanya kuwa jiji lake kuu. (2 Samweli 5:6, 7, 9) Pia, alilipeleka Sanduku takatifu huko. (2 Samweli 6:17) Kwa kuwa Sanduku lilihusianishwa na kuwapo kwa Yehova, Sayuni liliitwa mahali pa makao ya Mungu, nalo linafaa kabisa kuwakilisha mbinguni.—Kutoka 25:22; Mambo ya Walawi 16:2; Zaburi 9:11; Ufunuo 11:19.