Maelezo ya Chini
a Ingawa tafsiri nyingi za Biblia zinatafsiri neno la Kiebrania ’eʹrets kuwa “nchi” badala ya “dunia,” si lazima neno ’eʹrets kwenye Zaburi 37:11, 29 litafsiriwe tu nchi ambayo taifa la Israeli lilipewa. Kitabu kimoja (Old Testament Word Studies) cha William Wilson kinafafanua neno ’eʹrets kuwa “dunia yote kwa jumla, kutia ndani sehemu zinazokaliwa na zile zisizokaliwa; neno hilo linapotumiwa katika maana isiyo pana linamaanisha sehemu fulani ya dunia, yaani, nchi fulani.” Hivyo, maana ya kwanza ya neno la Kiebrania ni sayari yetu, yaani, dunia.—Ona gazeti la Mnara wa Mlinzi la Kiingereza au la Kifaransa la Januari 1, 1986, ukurasa wa 31.