Maelezo ya Chini
c Nadhiri zifuatazo zinazomheshimu Mungu zinatumiwa ikiwa sheria za nchi zinaruhusu. Kwa ajili ya bwana-arusi: “Mimi [jina la bwana-arusi] nakuchukua wewe [jina la bibi-arusi] uwe mke wangu wa ndoa, nikupende na kukutunza sana kulingana na sheria ya kimungu iliyoonyeshwa katika Maandiko Matakatifu kwa ajili ya waume Wakristo, kwa muda wote ambao sisi wawili tutaishi pamoja duniani kulingana na mpango wa ndoa wa Mungu.” Kwa ajili ya bibi-arusi: “Mimi [jina la bibi-arusi] nakuchukua wewe [jina la bwana-arusi] uwe mume wangu wa ndoa, nikupende na kukutunza na kukuheshimu sana, kulingana na sheria ya kimungu iliyoonyeshwa katika Maandiko Matakatifu kwa ajili ya wake Wakristo, kwa muda wote ambao sisi wawili tutaishi pamoja duniani kulingana na mpango wa ndoa wa Mungu.”