Maelezo ya Chini
a Maandiko yanatumia neno “nuru” kwa njia mbalimbali za mfano. Kwa mfano, Biblia inamhusianisha Mungu na nuru. (Zaburi 104:1, 2; 1 Yohana 1:5) Mafundisho ya kiroho kutoka katika Neno la Mungu yanafananishwa na nuru. (Isaya 2:3-5; 2 Wakorintho 4:6) Wakati wa huduma yake duniani, Yesu alikuwa nuru. (Yohana 8:12; 9:5; 12:35) Wafuasi wa Yesu waliamriwa waache nuru yao iangaze.—Mathayo 5:14, 16.