Maelezo ya Chini
a Kama ile sala ya kielelezo ambayo Yesu alitoa, sala ya Kiyahudi pia ina ombi la kwamba jina la Mungu litakaswe. Ingawa kuna ubishi kuhusu ikiwa sala hiyo ya Kiyahudi ilianza wakati wa Kristo au hata mapema zaidi, hatupaswi kushangaa kwamba inafanana na ile sala ya kielelezo. Sala ya Yesu haikukusudiwa iwe mpya na ya pekee. Sala hizo mbili zilitegemea kabisa Maandiko ambayo Wayahudi wote walikuwa nayo wakati huo. Yesu alikuwa akiwatia moyo Wayahudi wenzake wasali mambo ambayo walipaswa kuwa wakisali kabla ya yeye kuja duniani.