Maelezo ya Chini
a Yesu alisema: “Lazima ninyi basi muwe wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.” (Mt. 5:48) Inaelekea alielewa kwamba hata wanadamu wasio wakamilifu wanaweza kuwa kamili, au wakamilifu kwa kadiri fulani. Tunaweza kutimiza amri ya kuwapenda wengine kutoka moyoni, na hivyo kumpendeza Mungu. Hata hivyo, Yehova ni mkamilifu katika maana kamili. Neno “utimilifu” linapotumiwa kumhusu, linahusisha pia ukamilifu.—Zab. 18:30.