Maelezo ya Chini
c Imeonekana kwamba kutotajwa tena kwa Yosefu katika masimulizi ya huduma ya Yesu ni jambo lenye kutokeza kwa sababu washiriki wengine wa familia ya Yesu, yaani, mama, ndugu na dada zake wanatajwa. Kwa mfano, katika karamu ya arusi huko Kana, Maria anatajwa na hata inaonekana alikuwa na daraka fulani, lakini Yosefu hatajwi. (Yohana 2:1-11) Katika kisa kingine, tunaona watu katika mji wa nyumbani wa Kristo wakimtaja Yesu kuwa “mwana wa Maria” wala si mwana wa Yosefu.—Marko 6:3.