Maelezo ya Chini
b Tafsiri ya Septuajinti inakazia jinsi Yona alivyolala fofofo kwa kusema kwamba alikuwa akikoroma. Hata hivyo, badala ya kuona usingizi wa Yona kuwa ishara ya kutojali, tunapaswa kukumbuka kwamba nyakati fulani watu walioshuka moyo wanapatwa na usingizi. Yesu alipokuwa na uchungu mwingi katika bustani ya Gethsemane, Petro, Yakobo, na Yohana walikuwa “wakisinzia kwa huzuni.”—Luka 22:45.