Maelezo ya Chini
a Mtu aliyemtayarishia mgeni mwana-kondoo wa kula alionyesha sifa ya ukaribishaji-wageni. Lakini mtu aliyeiba mwana-kondoo alifanya uhalifu, na hivyo aliadhibiwa kwa kulipa kondoo wanne. (Kutoka 22:1) Kwa maoni ya Daudi, mtu huyo tajiri ambaye alichukua mwana-kondoo wa maskini hakuwa na huruma. Kwa hiyo, tajiri huyo aliiba mnyama wa yule mwanamume maskini ambaye huenda angeandalia familia yake maziwa na manyoya na ambaye hata angezaa kundi kubwa la kondoo.