Maelezo ya Chini
b Andiko la Mambo ya Walawi 19:18 linasema hivi: “Usilipize kisasi wala usiwe na kinyongo juu ya wana wa watu wako; nawe mpende mwenzako kama wewe mwenyewe.” Viongozi wa dini ya Kiyahudi waliamini kwamba maneno “wana wa watu wako” na “mwenzako” yaliwahusu Wayahudi tu. Sheria iliwaagiza Waisraeli wajitenge na mataifa mengine. Hata hivyo, sheria haikuunga mkono maoni yaliyoenezwa na viongozi wa kidini wa karne ya kwanza, ya kwamba watu wote ambao hawakuwa Wayahudi walikuwa maadui na hivyo walipaswa kuchukiwa wakiwa mtu mmoja-mmoja.