Maelezo ya Chini
a Wasomi fulani wa Biblia wanafikiri kwamba huenda maneno “ngozi kwa ngozi” yanamaanisha kwamba Ayubu angekuwa tayari kuruhusu kwa uchoyo watoto na wanyama wake wapoteze ngozi zao, au uhai, ikiwa tu yeye angeendelea kuwa na ngozi yake, au uhai. Wengine wanafikiri maneno hayo yanakazia kwamba mtu angekuwa tayari kupoteza sehemu fulani ya ngozi ikiwa hilo lingemaanisha kuokoa uhai wake. Kwa mfano, mtu anaweza kuinua mkono wake ili ajikinge asipigwe kichwa, na hivyo kupoteza sehemu fulani ya ngozi yake. Haidhuru maneno hayo ya mfano yana maana gani, bila shaka yanamaanisha kwamba Ayubu alikuwa tayari kutoa kila kitu ili aendelee kuwa hai.