Maelezo ya Chini
a Mazungumzo ya Yesu na Petro yalihusu kumtambua Kristo na jukumu lake, na si kuhusu jukumu ambalo Petro angetimiza. (Mathayo 16:13-17) Baadaye, Petro mwenyewe alisema kwamba Yesu ndiye mwamba ambao juu yake kutaniko lingejengwa. (1 Petro 2:4-8) Mtume Paulo alithibitisha kuwa Yesu, wala si Petro, ndiye “jiwe la msingi la pembeni” la kutaniko la Kikristo.—Waefeso 2:20.