Maelezo ya Chini
b Yesu na mitume walionya kwamba kutaniko la Kikristo lingevamiwa na watu ambao wangefundisha mafundisho ya uasi. (Mathayo 13:24-30, 36-43; 2 Timotheo 4:3; 2 Petro 2:1; 1 Yohana 2:18) Maneno hayo yalitimia wakati kanisa, au kutaniko, la karne ya pili lilipoanza kukubali mapokeo ya kipagani na kuchanganya mafundisho ya Biblia na falsafa za Wagiriki.