Maelezo ya Chini
d Shasta wa Kwanza alikuwa na hisia zilizobadilika-badilika na hasira yenye jeuri. Herodoto, mwanahistoria Mgiriki, aliandika mambo fulani ambayo Shasta alifanya wakati wa vita vyake na Wagiriki yanayoonyesha hisia za mfalme huyo. Mfalme aliagiza daraja la muda la meli zilizounganishwa lijengwe ili kuvuka mlango wa bahari wa Hellespont. Dhoruba ilipofagilia mbali daraja hilo, Shasta aliagiza mafundi wake wakatwe vichwa na watu wake “waadhibu” Hellespont kwa kupiga maji huku ujumbe wa matusi ukisomwa kwa sauti kubwa. Pindi hiyo, mwanamume fulani tajiri alipoomba mwana wake asiandikishwe jeshini, Shasta aliagiza kijana huyo akatwe vipande viwili na mwili wake uwekwe mahali palipo wazi ili kuwa onyo kwa wengine.