Maelezo ya Chini
e Kuna mabamba ya mambo ya kibiashara kuhusu kipindi chote cha watawala wa Milki Mpya ya Babiloni. Miaka ya utawala wa wafalme hao inapojumlishwa na kuihesabu kurudi nyuma, kuanzia wakati wa Nabonido, mtawala wa mwisho wa Milki Mpya ya Babiloni, inaonekana kwamba jiji la Yerusalemu liliharibiwa mwaka wa 587 K.W.K. Hata hivyo, njia hiyo ya kuhesabu inaweza tu kuwa sahihi ikiwa kila mfalme alianza kutawala mwaka uleule ambao mfalme aliyemtangulia aliondoka, bila kipindi fulani kupita kati ya watawala hao.