Maelezo ya Chini
a Waandishi wa kale walibadili andiko hilo kuwa “nafsi yangu,” kana kwamba linamrejelea Yeremia. Ni wazi waliamini kwamba ni ukosefu wa heshima kumrejelea Mungu kuwa nafsi, neno ambalo Biblia inatumia kumaanisha viumbe walio duniani. Lakini mara nyingi Biblia inaeleza kumhusu Mungu katika njia ambayo wanadamu wanaweza kuelewa. Kwa sababu neno “nafsi” linaweza kumaanisha “uhai wetu,” hivyo basi maneno “nafsi yako” linamaanisha “wewe.”