Maelezo ya Chini
a Kama tunavyosoma katika Matendo 20:29 na 30, Paulo alisema kwamba ‘watu wangesimama kutoka katika makutaniko ya Kikristo na kusema mambo yaliyopotoka ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao wenyewe.’ Historia inathibitisha kwamba baada ya muda kulikuwa na tofauti kubwa kati ya makasisi na watu wa kawaida. Kufikia karne ya tatu W.K., makasisi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo walidhihirisha wazi kwamba walikuwa yule “mtu wa uasi-sheria.”—Tazama Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 1990, ukurasa wa 10-14.