Maelezo ya Chini
a Wasomi fulani wanasema huenda ndugu za Yosefu walifikiri zawadi ambayo baba yao alimpa Yosefu ilionyesha kwamba alikusudia kumpa mvulana huyo haki ya kuwa mzaliwa wa kwanza. Walijua Yosefu alikuwa mwana wa kwanza wa mke aliyependwa sana na Yakobo, mke aliyekusudia kumwoa kwanza. Pia, mwana wa kwanza wa Yakobo, Rubeni, alikuwa amelala na suria wa baba yake, na hivyo kumkosea heshima baba yake jambo lililofanya apoteze haki ya kuwa mzaliwa wa kwanza.—Mwanzo 35:22; 49:3, 4.