Maelezo ya Chini
a Inapendeza kuona jinsi ambavyo Yesu aliorodhesha mambo alipotumia mifano ambayo ilikuwa sehemu ya ishara ya kuwapo kwake. Kwanza, alizungumzia “mtumwa mwaminifu na mwenye busara,” kikundi kidogo cha ndugu watiwa mafuta ambao wangeongoza. (Mt. 24:45-47) Kisha, alitoa mifano ambayo iliwahusu hasa wale wote wenye tumaini la kwenda mbinguni. (Mt. 25:1-30) Mwishowe, alizungumzia wale wenye tumaini la kuishi duniani ambao wangewategemeza ndugu za Kristo. (Mt. 25:31-46) Vivyo hivyo, utimizo wa kisasa wa unabii wa Ezekieli unawahusu wale walio na tumaini la kwenda mbinguni. Ingawa kwa kawaida ufalme wa makabila kumi haufananishi wale walio na tumaini la kuishi duniani, kuunganishwa kunakozungumziwa katika unabii huo kunatukumbusha umoja uliopo kati ya wale walio na tumaini la kuishi duniani na wale walio na tumaini la kwenda mbinguni.