Maelezo ya Chini
a Baadhi ya wasomi wa Biblia wanasema kwamba Yuda alinukuu maneno hayo kutoka kwenye kitabu cha hekaya kinachoitwa Kitabu cha Enoko, ambacho kina habari za kubuniwa kumhusu Enoko. Kitabu hicho kimenukuu kwa usahihi unabii wa Enoko, lakini huenda unabii huo ulitolewa kwenye chanzo cha kale ambacho sasa hakipo kama vile nakala ya maandishi au masimulizi. Huenda Yuda alitumia chanzo hichohicho au alijifunza kuhusu Enoko kupitia Yesu ambaye aliona maisha ya Enoko kutoka Mbinguni.