Maelezo ya Chini
b Sara alikuwa dada nusu wa Abrahamu. Tera alikuwa baba yao wote wawili, lakini walikuwa na mama tofauti. (Mwanzo 20:12) Ingawa ndoa za aina hiyo hazikubaliki leo, ni muhimu kukumbuka kwamba mambo yalikuwa tofauti nyakati hizo. Wanadamu walikuwa karibu zaidi na ukamilifu ambao Adamu na Hawa waliupoteza. Kwa kuwa watu hao walikuwa na afya nzuri, ndoa za watu wa ukoo wa karibu hazikuwa na hatari za kinasaba zitokanazo na kuoa mtu wa ukoo. Hata hivyo, miaka 400 hivi baadaye, urefu wa maisha ulikuwa sawa na ilivyo kwa wakati wetu. Wakati huo, Sheria ya Musa ilikataza mahusiano yoyote ya kingono kati ya ndugu wa karibu wa ukoo.—Mambo ya Walawi 18:6.