Maelezo ya Chini
a Watu wengi hawatambui kwamba katika Biblia fulani mistari ya Yohana 7:53–8:11 haikuwa sehemu ya maandishi ya awali yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Kwa msingi wa mistari hiyo, wengine wamedai kwamba ni mtu asiye na dhambi tu ndiye anayeweza kumwona mwingine kuwa mwenye hatia ya uzinzi. Lakini sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli ilisema hivi: “Ikiwa mwanamume atapatikana akilala na mwanamke aliye na mume, wote wawili watauawa pamoja.”—Kum. 22:22.