Maelezo ya Chini
a Huenda baadhi ya akina mama wanaopata ugonjwa wa kushuka moyo baada ya kujifungua wakashindwa kujenga uhusiano wa karibu na watoto wao. Hata hivyo, hawapaswi kujilaumu. Kulingana na Taasisi ya Kitaifa ya Afya ya Akili nchini Marekani (NIMH), inaelekea ugonjwa wa kushuka moyo baada ya kujifungua “unasababishwa na matatizo ya kimwili na ya kihisia . . . na hautokani na mambo ambayo mama anafanya au ambayo hafanyi.” Ili kupata habari zaidi kuhusu ugonjwa huo, soma makala “Kuelewa Mshuko wa Moyo Baada ya Kujifungua” katika gazeti la Amkeni! la Juni 8, 2003.