Maelezo ya Chini
b Kutuma ujumbe mchafu (Sexting), kunatia ndani kutuma ujumbe wa maneno, picha, na video za ngono kupitia simu ya mkononi. Ikitegemea na hali ambazo zimehusika, hatua ya kihukumu inaweza kuchukuliwa. Katika visa fulani vijana ambao hawajatimiza umri wa miaka 18, ambao wamewatumia wengine ujumbe mchafu wameshtakiwa kwa makosa ya kingono. Kwa habari zaidi, nenda kwenye Tovuti ya jw.org/sw na usome makala yenye kichwa, “Vijana Huuliza—Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kutuma Ujumbe Mchafu?” (Tafuta kwenye MAFUNDISHO YA BIBLIA > MATINEJA.) Au tazama makala yenye kichwa, “Jinsi ya Kuzungumza na Kijana Wako Kuhusu Kutuma Ujumbe Mchafu” iliyo katika gazeti la Amkeni! toleo la Novemba 2013, uku. 4-5.