Maelezo ya Chini
a Tunafurahia watu wanapoitikia vizuri habari njema, na tunavunjika moyo wanaposhindwa kufanya hivyo. Vipi ikiwa mwanafunzi wa Biblia unayemsaidia hafanyi maendeleo? Au vipi ikiwa wewe binafsi hujawahi kumsaidia mtu yeyote afikie hatua ya ubatizo? Je, ufikie mkataa kwamba umeshindwa kutimiza kazi ya kufanya wanafunzi? Katika makala hii, tutaona kwa nini tunaweza kufanikiwa katika huduma yetu na kupata shangwe licha ya itikio tunalopata.