Maelezo ya Chini
a Timotheo alikuwa mhudumu wa habari njema mwenye uzoefu mwingi. Hata hivyo, mtume Paulo alimtia moyo azidi kufanya maendeleo ya kiroho. Kwa kufuata shauri la Paulo, Timotheo angetumiwa zaidi na Yehova na angewasaidia zaidi ndugu na dada zake. Je, kama Timotheo, unatamani kumtumikia Yehova na waabudu wenzako kikamili zaidi? Bila shaka, ungependa kufanya hivyo. Ni malengo gani yatakayokusaidia kufanya hivyo? Na ni mambo gani yanayohusika katika kujiwekea na kutimiza malengo hayo?