Maelezo ya Chini
a Yehova ametupatia tumaini zuri ajabu la wakati ujao. Tumaini hilo linatusaidia kuwa na maisha yenye kusudi na kuepuka kukazia fikira matatizo tunayokabili sasa. Linatutia nguvu ili tuendelee kuwa waaminifu licha ya hali ngumu tunazokabili. Pia linaweza kutulinda ili tusinaswe na mawazo yanayoweza kupotosha njia yetu ya kufikiri. Kama tutakavyojifunza katika makala hii, hizo ni sababu nzuri za kuendelea kudumisha tumaini letu la Kikristo likiwa imara.