Maelezo ya Chini
a Andiko la mwaka lenye kuimarisha imani limechaguliwa kwa ajili ya mwaka wa 2023: “Kiini hasa cha neno lako ni kweli.” (Zab. 119:160) Bila shaka, unakubaliana na maneno hayo. Lakini watu wengi hawaamini kwamba Biblia inasema ukweli na kwamba inaweza kutupatia mwongozo unaotegemeka. Katika makala hii, tutachunguza mambo matatu yanayoweza kutusaidia kuwasadikisha wale wenye mioyo minyoofu kwamba wanaweza kuitumaini Biblia na ushauri wake.