Maelezo ya Chini
a Sisi sote tunaomwabudu Yehova tunajitahidi kusoma Neno lake kila siku. Wengine wengi husoma Biblia pia; ingawa hivyo, kwa kweli hawaelewi yale wanayosoma. Hivyo ndivyo ilivyokuwa pia kwa baadhi ya watu katika siku za Yesu. Tunapochunguza mambo ambayo Yesu aliwaambia wale waliosoma Neno la Mungu, tutapata masomo ambayo yanaweza kutusaidia tunufaike zaidi tunaposoma Biblia.