Maelezo ya Chini
b Biblia inataja pindi mbili ambazo wanyama walitolewa dhabihu kwa Yehova nyikani. Pindi ya kwanza ni wakati ukuhani ulipoanzishwa rasmi; na pindi ya pili ni siku ya Pasaka. Matukio hayo mawili yalifanyika mwaka wa 1512 K.W.K., mwaka wa pili baada ya Waisraeli kuondoka Misri.—Law. 8:14–9:24; Hes. 9:1-5.