Maelezo ya Chini
d Mfalme Asa alitenda dhambi nzito. (2 Nya. 16:7, 10) Hata hivyo, Biblia inasema Asa alifanya mambo yaliyo sawa machoni pa Yehova. Ingawa mwanzoni alikataa kurekebishwa, inawezekana kwamba baadaye alitubu. Kwa ujumla, sifa zake nzuri zilikuwa nyingi kuliko mambo mabaya aliyofanya. Jambo muhimu ni kwamba Asa alimwabudu tu Yehova na alijitahidi kuondoa ibada ya sanamu katika ufalme wake.—1 Fal. 15:11-13; 2 Nya. 14:2-5.