Maelezo ya Chini
a Waisraeli wengi ambao waliona miujiza ya Yehova katika Bahari Nyekundu walikufa kabla ya kuiona Nchi ya Ahadi. (Hes. 14:22, 23) Yehova alisema kwamba wanaume wenye umri wa miaka 20 na zaidi wangekufa nyikani. (Hes. 14:29) Hata hivyo, Yoshua, Kalebu, na wengi kati ya wale wenye umri chini ya miaka 20, na kabila la Lawi walifaulu kuona Yehova akitimiza ahadi yake wakati taifa la Israeli lilipovuka Mto Yordani na kuingia Kanaani.—Kum. 1:24-40.